Showing posts with label Maswali na Majibu. Show all posts
Showing posts with label Maswali na Majibu. Show all posts

Saturday, April 9, 2016

Mchumba wangu hatakiwi kwetu nifanyaje?


Habari zenu Wanajamvi,
Natumaini wote ni wazima wa afya njema,  Nia na madhumuni ya kuandika waraka huu ni kuomba ushauri kwani naamini penye wengi pana mengi......... Nina  mpenzi wa miaka minne  toka tuanze mahusiano yetu na kama ilivyo kawaida mkiwa kwenye mahusiano lazima muwe na mipango mingi ya maisha yenu ya kifamilia hapo baadae  hasa ndoa pamoja......

Kwa kuwa nampenda mpenzi wangu nikaona si vibaya kama nikienda nae nyumbani waanze kumzoea na yeye kuwafahamu ndugu zangu wengine.....

Sasa baada ya kumpeleka nyumbani siku  nikawekewa kikao cha familia na kuambiwa kuwa mtu nilienae hanifai, ana background mbaya na hawapo tayari kuona mimi nikimuoa huyo binti.....

Nilijitetea sana kumsafisha mpenzi wangu aonekane si mtu mbaya kama wanavyosema ila juhudi zangu ziligonga mwamba kabisa, na kuniambia hawamtani na nisiende nae tena nyumbani siku nyingine!!!1

Naomben ushauri, Mpenzi wangu bado napmpenda.......je nimwambie mpenzi wangu hali halisi ilivyo? Maana toka siku hiyo akiniambia habari za yeye walivyompokea nyumbani nafsi yangu inakuwa inanisuta

Uncle J Dar

Wednesday, February 3, 2016

Mgeni wa Mke wangu(Mwanaume), anahudumiwa na mke wangu zaidi yangu


Habari zenu wanajamvi,

Naombei msaada katika hili, rafiki yangu ameoa na ana watoto wawili chini ya miaka mitano,majuzi mkewe kamkaribisha mwanaume mwenye mtoto toka kijijini kwao Kwediboma,Handeni ili aje hapa Tanga mjini kwa ajili ya matibabu ya mwanawe.

Jamaa anaishi nyumba ya vyumba viwili na sebule na huyo mgeni wa mke wake amepewa chumba chake,jamaa kinachomuumiza kichwa ni mwenendo wa mkewe kumuandalia maji ya kuoga na kumuhandle huyo mgeni wa kiume kwa heshima kubwa bila yeye mumewe kutowahi kupata huduma hizo siku za nyuma.

Ameshamwambia mkewe kuwa hamhitaji mgeni huyo nyumbani kwake,ila mkewe amejitetetea kuwa jamaa hana mwenyeji mwingine hapa mjini.

Kesho ni siku ya jamaa(mgeni wa huyo mwanamke) kwenda kliniki Bombo hospitali kwa ajili ya upasuaji wa henia ya mwanawe,na hapo ndipo dereva la daladala anapopata shaka zaidi ya kukosa kumuona mkewe kwa kuwa atakuwa bize kumpelekea chakula jamaa na mwanaye hospitalini.

Dereva wa daladala amechanganyikiwa,anaomba ushauri wenu afanye nini? Yaani mpaka mishipa ya kichwa imemtoka na anaonekana kukosa amani kabisa.